dcsimg

Fisi-maji ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fisi-maji ni wanyama wa maji baridi au wa bahari (spishi mbili) wa nusufamilia Lutrinae katika familia Mustelidae. Wanyawa hawa wana mwili mrefu na mwembamba wenye mkia mrefu na manyoyo laini. Fisi-maji hushinda takriban maisha yao yote majini au baharini. Huogelea kwa kutumia miguu yao yenye ngozi kati ya vidole. Mkia hutumika kwa kupiga mbio umbali mdogo. Spishi za maji baridi hula samaki hasa lakini pia vyura, kasa wa maji baridi, mabata wadogo, panya na wadudu iwapo hakuna samaki wengi. Fisi-bahari wanastahabu invertebrata wa bahari kama kaa, kamba, uduvi, samakigamba, konokono wa bahari na chani, lakini samaki pengine pia. Huzaa watoto 1-5. Spishi za maji baridi huchimba au hutafuta tundu au mti uliobopa mara nyingi lakini fisi-bahari huzaa majini.

Spishi za Afrika

Spishi za mabara mengine

Spishi za kabla ya historia

  • Algarolutra majori (Pleistocene ya Korsika na Sardinia)
  • Sardolutra ichnusae (Mwisho wa Pleistocene ya Sardinia)
  • Megalenhydris barbaricina (Mwisho wa Pleistocene ya Sardinia)

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Fisi-maji: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fisi-maji ni wanyama wa maji baridi au wa bahari (spishi mbili) wa nusufamilia Lutrinae katika familia Mustelidae. Wanyawa hawa wana mwili mrefu na mwembamba wenye mkia mrefu na manyoyo laini. Fisi-maji hushinda takriban maisha yao yote majini au baharini. Huogelea kwa kutumia miguu yao yenye ngozi kati ya vidole. Mkia hutumika kwa kupiga mbio umbali mdogo. Spishi za maji baridi hula samaki hasa lakini pia vyura, kasa wa maji baridi, mabata wadogo, panya na wadudu iwapo hakuna samaki wengi. Fisi-bahari wanastahabu invertebrata wa bahari kama kaa, kamba, uduvi, samakigamba, konokono wa bahari na chani, lakini samaki pengine pia. Huzaa watoto 1-5. Spishi za maji baridi huchimba au hutafuta tundu au mti uliobopa mara nyingi lakini fisi-bahari huzaa majini.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri