dcsimg

Mzabibu ( Suaíli )

fornecido por wikipedia emerging languages

Mizabibu ni spishi mbalimbali za jenasi Vitis katika familia Vitaceae; spishi kuu ni Vitis vinifera. Matunda yao huitwa zabibu ambazo hutumika kwa kutengeneza mvinyo. Mmea wa mzabibu ni mtambazi unaopanda juu ya mimea mingine au miwamba msituni, juu ya kuta katika bustani au kwa kamba shambani. Maua na matunda yamo kwa kicha.

Mzabibu katika Biblia

Kwa kuwa mzabibu ulikuwa kilimo muhimu cha Israeli tangu watu wa taifa hilo walipohamia nchi hiyo, mti huo unatajwa mara nyingi katika Biblia hadi Agano Jipya. Hasa katika Injili ya Yohane, Yesu alijiita mzabibu wa kweli ambao waamini wake ni matawi yanayoweza kuzaa ikiwa tu yanadumu ndani ya shina na kufyonza utomvu wake.

Katika karamu ya mwisho Yesu pia alitumia divai iliyotokana na zabibu kama ishara ya damu yake iliyotakiwa kumwagwa msalabani kwa maondoleo ya dhambi.

Picha

licença
cc-by-sa-3.0
direitos autorais
Waandishi wa Wikipedia na wahariri
original
visite a fonte
site do parceiro
wikipedia emerging languages

Mzabibu: Brief Summary ( Suaíli )

fornecido por wikipedia emerging languages

Mizabibu ni spishi mbalimbali za jenasi Vitis katika familia Vitaceae; spishi kuu ni Vitis vinifera. Matunda yao huitwa zabibu ambazo hutumika kwa kutengeneza mvinyo. Mmea wa mzabibu ni mtambazi unaopanda juu ya mimea mingine au miwamba msituni, juu ya kuta katika bustani au kwa kamba shambani. Maua na matunda yamo kwa kicha.

licença
cc-by-sa-3.0
direitos autorais
Waandishi wa Wikipedia na wahariri
original
visite a fonte
site do parceiro
wikipedia emerging languages