Vipiri au vifutu ni spishi za nyoka wenye sumu katika familia Viperidae. Spishi nyingine huitwa bafe au moma pia.
Nyoka hawa sio warefu sana lakini wanene kwa kulinganisha na nyoka wengine na wana kichwa kipana kwa umbo wa pembetatu na mkia mfupi. Kwa kawaida magamba yao yana miinuko ambayo inaweza kuwa kama miiba. Miboni ya macho ni kama chanjo za wima ikiwa imefungwa kwa kiasi.
Waking'ata vipiri huingiza sumu katika mwili kupitia chonge mbili zenye mifereji. Mdomo ukiwa umefungwa chonge hizi zinalala kutegemea dari lake. Lakini iwapo kipiri akifungua mdomo chonge huduru mbele ili kudunga. Misuli inayofunga mdomo inakamua pia sumu kutoka tezi.
Vipiri sio wepesi sana na kwa hivyo wako hatari. Kwa sababu wana rangi za kamafleji hukaa bila kusogea hata kama adui anakaribia. Mtu anaweza kumkanyaga kipiri bila kumwona kisha kuumwa na kudungwa sumu. Lakini wakati mwingine kipiri anauma bila kuingiza sumu.
Sumu ya vipiri ina vimeng'enya vingi vinavyomeng'enya proteini (proteasi). Mchakato huu unasababisha maumivu makali, uvimbe na kuoza kwa tishu. Hata akipona mwathirika atakaa na kovu.
Vipiri au vifutu ni spishi za nyoka wenye sumu katika familia Viperidae. Spishi nyingine huitwa bafe au moma pia.
Nyoka hawa sio warefu sana lakini wanene kwa kulinganisha na nyoka wengine na wana kichwa kipana kwa umbo wa pembetatu na mkia mfupi. Kwa kawaida magamba yao yana miinuko ambayo inaweza kuwa kama miiba. Miboni ya macho ni kama chanjo za wima ikiwa imefungwa kwa kiasi.
Waking'ata vipiri huingiza sumu katika mwili kupitia chonge mbili zenye mifereji. Mdomo ukiwa umefungwa chonge hizi zinalala kutegemea dari lake. Lakini iwapo kipiri akifungua mdomo chonge huduru mbele ili kudunga. Misuli inayofunga mdomo inakamua pia sumu kutoka tezi.
Vipiri sio wepesi sana na kwa hivyo wako hatari. Kwa sababu wana rangi za kamafleji hukaa bila kusogea hata kama adui anakaribia. Mtu anaweza kumkanyaga kipiri bila kumwona kisha kuumwa na kudungwa sumu. Lakini wakati mwingine kipiri anauma bila kuingiza sumu.
Sumu ya vipiri ina vimeng'enya vingi vinavyomeng'enya proteini (proteasi). Mchakato huu unasababisha maumivu makali, uvimbe na kuoza kwa tishu. Hata akipona mwathirika atakaa na kovu.