dcsimg

Kanghagha ( swahili )

fornì da wikipedia emerging languages

Kanghagha au zogoyogo ni ndege wa familia Leiotrichidae. Wanafanana na mikesha wa familia Turdidae. Wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika na Asia. Spishi za Afrika zina rangi za kahawa, nyeusi, kijivu na nyeupe, lakini spishi nyingi za Asia zina rangi kali pia kama nyekundu na njano. Takriban spishi zote huenda kwa makundi wakiwasiliana kwa sauti. Mara kwa mara hupiga kelele sana, kwa sababu yake huitwa mpayupayu pia (“babbler” au “chatterer” kwa Kiingereza). Hula wadudu hasa lakini beri pia; spishi kubwa hula mijusi na panya wadogo na spishi kadhaa hula beri tu. Hulijenga tago lao kwa vitawi na kulificha katika vichaka vizitu. Jike huyataga mayai 2-5. Spishi kadhaa hujenga tago kwa kundi; jike mmoja tu hutaga mayai na ndege wengine husaidia kuwalinda makinda na kuwaletea chakula.

Spishi za Afrika

Spishi za Asia

Picha

licensa
cc-by-sa-3.0
drit d'autor
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Kanghagha: Brief Summary ( swahili )

fornì da wikipedia emerging languages

Kanghagha au zogoyogo ni ndege wa familia Leiotrichidae. Wanafanana na mikesha wa familia Turdidae. Wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika na Asia. Spishi za Afrika zina rangi za kahawa, nyeusi, kijivu na nyeupe, lakini spishi nyingi za Asia zina rangi kali pia kama nyekundu na njano. Takriban spishi zote huenda kwa makundi wakiwasiliana kwa sauti. Mara kwa mara hupiga kelele sana, kwa sababu yake huitwa mpayupayu pia (“babbler” au “chatterer” kwa Kiingereza). Hula wadudu hasa lakini beri pia; spishi kubwa hula mijusi na panya wadogo na spishi kadhaa hula beri tu. Hulijenga tago lao kwa vitawi na kulificha katika vichaka vizitu. Jike huyataga mayai 2-5. Spishi kadhaa hujenga tago kwa kundi; jike mmoja tu hutaga mayai na ndege wengine husaidia kuwalinda makinda na kuwaletea chakula.

licensa
cc-by-sa-3.0
drit d'autor
Waandishi wa Wikipedia na wahariri