Mtipitipi (pia mturituri, mchechepwa, kikwajuzi, kitimutimu, sindamu na songu; kwa lugha ya kisayansi Abrus precatorius) ni mmea mtambaa wa familia Fabaceae. Mbegu zake nyekundu na nyeusi huitwa matipitipi na hutumika kama shanga.
Matipitipi yana sumu ndani yao inayoitwa abrini na iliyo na mnasaba na risini, sumu ya mbegu za mbarika. Ganda la mbegu ni gumu sana. Kwa hivyo kumeza tipitipi lisilovunjika hakuleti shida, kwa sababu mbegu inanyewa bila badiliko. Lakini kutafuna na kumeza tipitipi moja tu kunaweza kumwua mtu mzima. Udungaji wa kiasi kidogo cha abrini unamwua mtu pia. Kwa hivyo kutoboa matipitipi na kuyatumia kama shanga ni hatari sana.
Mtipitipi (pia mturituri, mchechepwa, kikwajuzi, kitimutimu, sindamu na songu; kwa lugha ya kisayansi Abrus precatorius) ni mmea mtambaa wa familia Fabaceae. Mbegu zake nyekundu na nyeusi huitwa matipitipi na hutumika kama shanga.
Matipitipi yana sumu ndani yao inayoitwa abrini na iliyo na mnasaba na risini, sumu ya mbegu za mbarika. Ganda la mbegu ni gumu sana. Kwa hivyo kumeza tipitipi lisilovunjika hakuleti shida, kwa sababu mbegu inanyewa bila badiliko. Lakini kutafuna na kumeza tipitipi moja tu kunaweza kumwua mtu mzima. Udungaji wa kiasi kidogo cha abrini unamwua mtu pia. Kwa hivyo kutoboa matipitipi na kuyatumia kama shanga ni hatari sana.