Lemuri-spoti (kutoka Kiingereza: sportive lemur) ni spishi za lemuri wa jenasi Lepilemur, jenasi pekee ya familia Lepilemuridae. Kama lemuri wote wanatokea Madagaska tu. Lemuri hawa ni wakubwa kiasi na wana manyoya kahawiakijivu kuelekea mekundu mgongoni na meupenjano chini. Urefu wa mwili wao ni sm 30-35 na mkia una urefu sawa. Uzito wao ni hadi g 900. Wana safu ya seli kama kioo (tapetum lucidum) mbele ya retina inayoakisi mwanga, kwa hivyo macho yao yana mng'ao (eyeshine). Hula majani hasa.
Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.
Lemuri-spoti (kutoka Kiingereza: sportive lemur) ni spishi za lemuri wa jenasi Lepilemur, jenasi pekee ya familia Lepilemuridae. Kama lemuri wote wanatokea Madagaska tu. Lemuri hawa ni wakubwa kiasi na wana manyoya kahawiakijivu kuelekea mekundu mgongoni na meupenjano chini. Urefu wa mwili wao ni sm 30-35 na mkia una urefu sawa. Uzito wao ni hadi g 900. Wana safu ya seli kama kioo (tapetum lucidum) mbele ya retina inayoakisi mwanga, kwa hivyo macho yao yana mng'ao (eyeshine). Hula majani hasa.