dcsimg

Chozi (ndege) ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Chozi ni ndege wadogo wa familia Nectariniidae. Spishi za jenasi kadhaa zinaitwa neli. Spishi nyingi sana zina rangi kali zinazong'aa juani kama metali. Manyoya ya kati ya mkia ni marefu sana katika spishi nyingine. Domo lao limepindika na hutumika kwa kutoa mbochi katika maua au wadudu katika matundu. Hula mbochi hasa na pengine maji ya matunda na wadudu pia. Wawindaji-buibui, ambao wamo pia katika familia hii, hula wadudu zaidi kuliko chozi.

Ndege hawa wanatokea kanda za tropiki na nusutropiki za Afrika, Asia na kaskazini mwa Australia. Tundu lao lina umbo la mfuko na limening'izika kwa vitawi vyembamba. Jike hutaga mayai 2-4.

Spishi za Afrika

Spishi za mabara mengine

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Chozi (ndege): Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Chozi ni ndege wadogo wa familia Nectariniidae. Spishi za jenasi kadhaa zinaitwa neli. Spishi nyingi sana zina rangi kali zinazong'aa juani kama metali. Manyoya ya kati ya mkia ni marefu sana katika spishi nyingine. Domo lao limepindika na hutumika kwa kutoa mbochi katika maua au wadudu katika matundu. Hula mbochi hasa na pengine maji ya matunda na wadudu pia. Wawindaji-buibui, ambao wamo pia katika familia hii, hula wadudu zaidi kuliko chozi.

Ndege hawa wanatokea kanda za tropiki na nusutropiki za Afrika, Asia na kaskazini mwa Australia. Tundu lao lina umbo la mfuko na limening'izika kwa vitawi vyembamba. Jike hutaga mayai 2-4.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri