dcsimg

Bweha (Canis) ( swahili )

fourni par wikipedia emerging languages

Bweha au mbweha wa jenasi Canis katika familia Canidae ni wanyama wadogo kiasi wanaofanana na mbwa. Mbwa-nyika (coyote, Canis latrans) huitwa “bweha wa Amerika” pengine[1], lakini kwa kawaida spishi nne tu katika jenasi Canis huitwa bweha.

Spishi hizi huwinda wanyama wadogo hadi wakubwa kiasi, kama mamalia wadogo, ndege na watambaachi. Ili kufanya hiyo husaidiwa na miguu yao mirefu na mikubwa na mifupa ya miguu iliyounganika. Sifa hizi zinawapa bweha uwezo wa kukimbia umbali mrefu na kudumisha mbio za hadi km 16 (maili 9.9) kwa saa kwa vipindi virefu. Bweha hukiakia wakati wa utusitusi wa alfajiri na machweo.

Kwa kawaida sehemu ya kijamii ni jozi inayokaa pamoja abadi na inayokinga eneo lake dhidi ya jozi nyingine wakifukuza washindani wanaovamia na kuweka mkojo na mavi kwa mipaka ya eneo kama landmarks. Ukubwa wa eneo hili unatosha hudhurio la wanyama wazima wachanga ambao wanakaa pamoja na wazazi wao mpaka wanapata maeneo wao. Bweha wanaweza kujikonga katika makundi madogo, kwa mfano ili kula mzoga, lakini kwa kawaida huwinda peke yao au kwa jozi.

Uainishaji na mahusiano

Kwa sababu bweha wa jenasi Canis na mbwa-nyika wanafanana, Lorenz Oken waliwaweka katika jenasi wao wenyewe Thos, kutoka jina la Kiyanuni kwa bweha θώς (Lehrbuch der Naturgeschichte, 1815, juzuu la tatu). Lakini wataalamu wachache wamemfuata.

Angel Cabrera, katika kitabu chake cha 1932 kuhusu wanyama wa Maroko, alijiuliza kwamba kuwepo kwa “cingulum” kwenye magego ya juu ya bweha na kutokuwepo kwa spishi nyingine za Canis kungesadikisha mgawanyiko wa jenasi Canis. Hatimaye alichagua kibadala cha jenasi isiyogawanyika na kurejea bweha kama Canis badala ya Thos[2].

Nadharia ya Oken ilikuwa imefufua mwaka 1914 na Edmund Heller ambaye alisadiki dhana jenasi tofauti. Majina ya Heller na designations alizozipatia spishi na nususpishi za bweha yanaendelea kutumika katika uainishaji wa kisasa ijapokuwa jenasi yao imebadilika tena kuwa Canis.

Tafiti za kisasa zimeonesha mahusiano baina ya spishi za bweha. Licha ya mishabaha yao bweha hawako kwenye tawi moja la mti wa familia Canidae. Bweha miraba na bweha mgongo-mweusi wamo mwenye tawi dhahiri la Canidae, ambapo bweha dhahabu ni karibu na mbwa-mwitu Habeshi (Canis simensis), mbwa-nyika (Canis latrans) na mbwa-mwitu wa Ulaya/mbwa-kaya (Canis lupus)[3]. Kwa sababu bweha miraba/mgongo-mweusi ni tofauti sana na bweha dhahabu (na pia wote wengine wa Canidae wanaofanana na mbwa-mwitu), imependekezwa kubadilisha jina la jenasi ya spishi hizi mbili hadi Lupulella kutoka Canis[4].

Hivi karibuni wataalamu wamefahamu kwamba bweha dhahabu wa Afrika ni spishi tofauti na yule wa Asia na Ulaya[5]. Jina “mbwa-mwitu dhahabu wa Afrika” linapendekezwa kwa spishi ya Afrika.

Spishi

Matumizi ya kale

 src=
Anubis na mumiani (maiti aliyehifadhiwa)

Mungu wa kale wa Misri, na wa chini duniani, Anubis, aliyezuia maiti wasioze, alionyeshwa kama mwanaume mwenye kichwa cha bweha.

Matumizi ya msimu

 src=
Bweha dhahabu
  • Taswira maarufu, japo si sahihi sana ya bweha kama wala mizoga kwa kiasi fulani imepelekea tafsiri mbaya.
  • Msemo ”umbweha” wakati fulani hutumika kuelezea kazi ifanywayo na mfanyakazi wa chini kwa ajili ya kuokoa mda ya mtu mkubwa (kwa mfano: mwanasheria mdogo anaweza kufanya kazi nyingi kwa niabu ya wakili). Hii imetokana na ile hadithi ya kwamba bweha humuongoza simba kwenye mawindo yake. Neno hili mli wakati mwingine hutumika kuelezea tabia ya mtu anayependa kujaribu kutumia na kufaidi mizoga ya mtu aliyepatwa na janga fulani. Mfano: kuvamia na kuiba kwenye kijiji kilicho kubwa na mafuriko na wakazi wake wamekimbia.
 src=
Pundamilia na bweha huko Kasoko ya Ngorongoro, Tanzania

Tanbihi

  1. Coyote (2004) by E.M. Gese & M. Bekoff
  2. Thos vs Canis
  3. Lindblad-Toh; et al. (2005). "Genome sequence, comparative analysis and haplotype structure of the domestic dog". Nature 438 (7069): 803–819. . .
  4. Dinets V. The Canis tangle: a systematics overview and taxonomic recommendations. Vavilovskii Zhurnal Genetiki i Selektsii – Vavilov Journal of Genetics and Breeding. 2015;19(3):286-291.
  5. Koepfli, K.-P.; Pollinger, J.; Godinho, R.; Robinson, J.; Lea, A.; Hendricks, S.; Schweizer, R. M.; Thalmann, O. et al. (2015-08-17). "Genome-wide Evidence Reveals that African and Eurasian Golden Jackals Are Distinct Species". Current Biology 25: 2158–65. . . http://www.cell.com/current-biology/abstract/S0960-9822%2815%2900787-3.
licence
cc-by-sa-3.0
droit d’auteur
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Bweha (Canis): Brief Summary ( swahili )

fourni par wikipedia emerging languages

Bweha au mbweha wa jenasi Canis katika familia Canidae ni wanyama wadogo kiasi wanaofanana na mbwa. Mbwa-nyika (coyote, Canis latrans) huitwa “bweha wa Amerika” pengine, lakini kwa kawaida spishi nne tu katika jenasi Canis huitwa bweha.

Spishi hizi huwinda wanyama wadogo hadi wakubwa kiasi, kama mamalia wadogo, ndege na watambaachi. Ili kufanya hiyo husaidiwa na miguu yao mirefu na mikubwa na mifupa ya miguu iliyounganika. Sifa hizi zinawapa bweha uwezo wa kukimbia umbali mrefu na kudumisha mbio za hadi km 16 (maili 9.9) kwa saa kwa vipindi virefu. Bweha hukiakia wakati wa utusitusi wa alfajiri na machweo.

Kwa kawaida sehemu ya kijamii ni jozi inayokaa pamoja abadi na inayokinga eneo lake dhidi ya jozi nyingine wakifukuza washindani wanaovamia na kuweka mkojo na mavi kwa mipaka ya eneo kama landmarks. Ukubwa wa eneo hili unatosha hudhurio la wanyama wazima wachanga ambao wanakaa pamoja na wazazi wao mpaka wanapata maeneo wao. Bweha wanaweza kujikonga katika makundi madogo, kwa mfano ili kula mzoga, lakini kwa kawaida huwinda peke yao au kwa jozi.

licence
cc-by-sa-3.0
droit d’auteur
Waandishi wa Wikipedia na wahariri