Mikonje, mikonge au panga ni spishi mbili za samaki wa baharini katika jenasi Chirocentrus ya familia Chirocentridae na oda Clupeiformes. Wana nasaba na dagaa.
Spishi zote mbili zina mwili uliorefuka na mataya yenye meno marefu makali ambayo huwezesha hamu yao kubwa, hasa kwa samaki wengine. Hufikia urefu wa m 1. Wana mbavu za rangi ya fedha na mgongo wa kibuluu.
Mikonje huvuliwa kwa kibiashara na kuuzwa wabichi au waliogandishwa.
Mikonje, mikonge au panga ni spishi mbili za samaki wa baharini katika jenasi Chirocentrus ya familia Chirocentridae na oda Clupeiformes. Wana nasaba na dagaa.
Spishi zote mbili zina mwili uliorefuka na mataya yenye meno marefu makali ambayo huwezesha hamu yao kubwa, hasa kwa samaki wengine. Hufikia urefu wa m 1. Wana mbavu za rangi ya fedha na mgongo wa kibuluu.
Mikonje huvuliwa kwa kibiashara na kuuzwa wabichi au waliogandishwa.