Vijogoo-shamba au bandabanda ni ndege wa familia Eurylaimidae. Wana domo pana na spishi nyingi zina rangi kali lakini zile za Afrika ni kahawia na nyeupe zenye michirizi myeusi isipokuwa kijogoo-shamba kijani ambaye ana rangi ya majani. Ndege hawa wanatokea misitu mizito. Hula matunda na hukamata wadudu kwa namna ya shore au chechele. Hupenda kuwa kwa makundi ya hadi kufikia ndege 20. Tago la vijogoo-shamba ni mjengo mkubwa (mpaka nusu mita) unaofungika na wenye mwingilio kwa upande wake. Limefumika kwa vitawi, manyasi na majani na kufunikika kwa tando za buibui, vigoga na kuvumwani. Jike huyataga mayai 1-3.
Vijogoo-shamba au bandabanda ni ndege wa familia Eurylaimidae. Wana domo pana na spishi nyingi zina rangi kali lakini zile za Afrika ni kahawia na nyeupe zenye michirizi myeusi isipokuwa kijogoo-shamba kijani ambaye ana rangi ya majani. Ndege hawa wanatokea misitu mizito. Hula matunda na hukamata wadudu kwa namna ya shore au chechele. Hupenda kuwa kwa makundi ya hadi kufikia ndege 20. Tago la vijogoo-shamba ni mjengo mkubwa (mpaka nusu mita) unaofungika na wenye mwingilio kwa upande wake. Limefumika kwa vitawi, manyasi na majani na kufunikika kwa tando za buibui, vigoga na kuvumwani. Jike huyataga mayai 1-3.