Wadudu mabawa-makubwa ni wadudu wakubwa kiasi hadi wakubwa sana wa oda Megaloptera (megalos = kubwa, ptera = mabawa) ambao wana mabawa makubwa yakilinganishwa na mwili wao. Wanaruka angani vigoigoi. Muda wa maisha ya wadudu wapevu ni mfupi, kwa kawaida siku chache (si zaidi ya wiki moja). Kwa kinyume lava huishi miaka 1-5 majini.
Oda hii ina familia mbili tu na spishi 8 zimeelezwa katika Afrika. Spishi kubwa kabisa duniani imefunuliwa huko Uchina. Haijapata jina la kisayansi lakini jina la Kiingereza ni Giant dobsonfly. Urefu wa mabawa pamoja ni sm 21.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.
Kamusi za Kiswahili hazina jina kwa mnyama huyu au wanyama hawa.
Wadudu mabawa-makubwa ni wadudu wakubwa kiasi hadi wakubwa sana wa oda Megaloptera (megalos = kubwa, ptera = mabawa) ambao wana mabawa makubwa yakilinganishwa na mwili wao. Wanaruka angani vigoigoi. Muda wa maisha ya wadudu wapevu ni mfupi, kwa kawaida siku chache (si zaidi ya wiki moja). Kwa kinyume lava huishi miaka 1-5 majini.
Oda hii ina familia mbili tu na spishi 8 zimeelezwa katika Afrika. Spishi kubwa kabisa duniani imefunuliwa huko Uchina. Haijapata jina la kisayansi lakini jina la Kiingereza ni Giant dobsonfly. Urefu wa mabawa pamoja ni sm 21.