dcsimg

Tupa (nyoka) ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Tupa ni spishi za nyoka za jenasi Gonionotophis katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu mwili wao una umbo wa tupa yenye pande tatu.

Nyoka hawa ni wafupi hadi warefu kiasi, kati ya sm 30 na 160. Kichwa cha spishi ndefu kinafanana na kile cha kambare. Kwa kawaida rangi yao ni nyeusi, kijivu au kahawia. Tupa kusi anaweza kuwa na mlia mweupe mgongoni.

Tupa huenda polepole na kuwinda usiku. Hula amfibia na watambaachi, ikijumuisha hata nyoka wengine.

Nyoka hawa hawana sumu na kwa kawaida hawang'ati wakishikwa na watu.

Spishi

Picha

Marejeo

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje

Crystal Clear app babelfish vector.svg Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tupa (nyoka) kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Tupa (nyoka): Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Tupa ni spishi za nyoka za jenasi Gonionotophis katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu mwili wao una umbo wa tupa yenye pande tatu.

Nyoka hawa ni wafupi hadi warefu kiasi, kati ya sm 30 na 160. Kichwa cha spishi ndefu kinafanana na kile cha kambare. Kwa kawaida rangi yao ni nyeusi, kijivu au kahawia. Tupa kusi anaweza kuwa na mlia mweupe mgongoni.

Tupa huenda polepole na kuwinda usiku. Hula amfibia na watambaachi, ikijumuisha hata nyoka wengine.

Nyoka hawa hawana sumu na kwa kawaida hawang'ati wakishikwa na watu.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri