Tupa ni spishi za nyoka za jenasi Gonionotophis katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu mwili wao una umbo wa tupa yenye pande tatu.
Nyoka hawa ni wafupi hadi warefu kiasi, kati ya sm 30 na 160. Kichwa cha spishi ndefu kinafanana na kile cha kambare. Kwa kawaida rangi yao ni nyeusi, kijivu au kahawia. Tupa kusi anaweza kuwa na mlia mweupe mgongoni.
Tupa huenda polepole na kuwinda usiku. Hula amfibia na watambaachi, ikijumuisha hata nyoka wengine.
Nyoka hawa hawana sumu na kwa kawaida hawang'ati wakishikwa na watu.
Tupa ni spishi za nyoka za jenasi Gonionotophis katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu mwili wao una umbo wa tupa yenye pande tatu.
Nyoka hawa ni wafupi hadi warefu kiasi, kati ya sm 30 na 160. Kichwa cha spishi ndefu kinafanana na kile cha kambare. Kwa kawaida rangi yao ni nyeusi, kijivu au kahawia. Tupa kusi anaweza kuwa na mlia mweupe mgongoni.
Tupa huenda polepole na kuwinda usiku. Hula amfibia na watambaachi, ikijumuisha hata nyoka wengine.
Nyoka hawa hawana sumu na kwa kawaida hawang'ati wakishikwa na watu.