Mng'ong'o )pia mng'ongo, mungango au mmorula; jina la kisayansi: Sclerocarya birrea) ni mti mkubwa wa savana. Matunda yake huitwa mang'ong'o au morula.
Mti huu haukuzwi kwa kawaida wala haukatwi ila huachwa porini kwa ajili ya matunda yake. Nyama ya matunda huliwa na kokwa mbichi zake pia. Matunda yanaweza kuchachuliwa ili kutengeneza pombe na hiyo inaweza kukenekwa ili kupata pombe kali (k.m. Amarula).
Juisi iliyochemshwa hutumika ili kukoleza uji uwe mtamu. Kokwa hupondwa ili kutengeneza keki na biskuti au kuweka supu rojorojo. Kokwa zinatoa mafuta pia yanayotumika kwa kupika na kupakia ngozi.
Mng'ong'o )pia mng'ongo, mungango au mmorula; jina la kisayansi: Sclerocarya birrea) ni mti mkubwa wa savana. Matunda yake huitwa mang'ong'o au morula.
Mti huu haukuzwi kwa kawaida wala haukatwi ila huachwa porini kwa ajili ya matunda yake. Nyama ya matunda huliwa na kokwa mbichi zake pia. Matunda yanaweza kuchachuliwa ili kutengeneza pombe na hiyo inaweza kukenekwa ili kupata pombe kali (k.m. Amarula).
Juisi iliyochemshwa hutumika ili kukoleza uji uwe mtamu. Kokwa hupondwa ili kutengeneza keki na biskuti au kuweka supu rojorojo. Kokwa zinatoa mafuta pia yanayotumika kwa kupika na kupakia ngozi.