Tandu-shamba ni aina za arithropodi wadogo katika ngeli Symphyla ya nusufaila Myriapoda. Hata kama wanafanana na tandu wa kawaida, inaonekana kwamba wana mnasaba zaidi na majongoo lakini uchanganuzi wa ADN umetoa matokeo yanayopingana. Hawa ni wanyama wadogo wenye mm 2-30. Mwili wao ni mwororo na unapenyeka kwa nuru. Hawana macho na hutumia vipapasio ili kusikia njia. Huonekana katika udongo mpaka kina cha sm 50. Hula dutu ya viumbehai lakini spishi kadhaa zinaweza kuharibu mimea ya shambani.
Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.
Tandu-shamba ni aina za arithropodi wadogo katika ngeli Symphyla ya nusufaila Myriapoda. Hata kama wanafanana na tandu wa kawaida, inaonekana kwamba wana mnasaba zaidi na majongoo lakini uchanganuzi wa ADN umetoa matokeo yanayopingana. Hawa ni wanyama wadogo wenye mm 2-30. Mwili wao ni mwororo na unapenyeka kwa nuru. Hawana macho na hutumia vipapasio ili kusikia njia. Huonekana katika udongo mpaka kina cha sm 50. Hula dutu ya viumbehai lakini spishi kadhaa zinaweza kuharibu mimea ya shambani.