Mijusi-islam ni mijusi wa familia Scincidae walio na ngozi laini inayong'aa. Spishi za jenasi Trachylepis huitwa magonda pia. Miguu ya mijusi hawa ni mifupi kwa kawaida na spishi nyingi zina miguu iliyopunguka au hazina miguu. Spishi hizi husongea kama nyoka.
Mijusi hawa ni wafupi (sm 5-6) hadi warefu kiasi (sm 60). Huishi kati ya mawe na miamba, katika vishimo, chini ya mchanga au takataka ya majani au juu ya miti. Chakula chao ni wadudu hasa lakini nyungunyungu, majongoo, konokono, mijusi wengine au vipanya pia.
Mijusi-islam ni mijusi wa familia Scincidae walio na ngozi laini inayong'aa. Spishi za jenasi Trachylepis huitwa magonda pia. Miguu ya mijusi hawa ni mifupi kwa kawaida na spishi nyingi zina miguu iliyopunguka au hazina miguu. Spishi hizi husongea kama nyoka.
Mijusi hawa ni wafupi (sm 5-6) hadi warefu kiasi (sm 60). Huishi kati ya mawe na miamba, katika vishimo, chini ya mchanga au takataka ya majani au juu ya miti. Chakula chao ni wadudu hasa lakini nyungunyungu, majongoo, konokono, mijusi wengine au vipanya pia.