Mpapai ni mti wa familia Caricaceae ambao unazaa mapapai.
Mti huo unatoka Meksiko lakini siku hizi hukuzwa kila mahali katika ukanda wa tropiki kwa sababu matunda yake hupendwa sana.
Ni mti mrefu wenye shina la urefu wa mita 5 mpaka 10, wenye majani yaliyojipanga yaliyojizungusha na kujishikiza juu kwenye shina la mti, shina kwa upande wa chini huwa na makovu mengi kuonesha sehemu ambayo majani yalikuwa. Majani ya mpapai ni makubwa sm 50 – 70 kwa upana, maua yake ni madogo na hutokea sehemu yalipochomoza majani, hutengeneza tunda papai lenye urefu wa sm 15- 45, na upana wa sm 10 – 30.
Mpapai ni mti wa familia Caricaceae ambao unazaa mapapai.
Mti huo unatoka Meksiko lakini siku hizi hukuzwa kila mahali katika ukanda wa tropiki kwa sababu matunda yake hupendwa sana.
Ni mti mrefu wenye shina la urefu wa mita 5 mpaka 10, wenye majani yaliyojipanga yaliyojizungusha na kujishikiza juu kwenye shina la mti, shina kwa upande wa chini huwa na makovu mengi kuonesha sehemu ambayo majani yalikuwa. Majani ya mpapai ni makubwa sm 50 – 70 kwa upana, maua yake ni madogo na hutokea sehemu yalipochomoza majani, hutengeneza tunda papai lenye urefu wa sm 15- 45, na upana wa sm 10 – 30.