dcsimg

Sengi ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Sengi, njule au isanje ni wanyama wadogo wa familia Macroscelididae. Jina la njule litumika kwa jenasi Rhynchocyon na isanje litumika kwa Petrodromus tetradactylus. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika maeneo mbalimbali. Sifa bainifu mno ya sengi ni pua yao refu sana ambayo wanaweza kuipota ili kutafuta chakula. Hii inafanana kidogo na mwiro wa tembo na ni chimbuko cha jina lao la Kiingereza "elephant shrew". Miguu yao ni mirefu kwa kulinganisha na huenda wakirukaruka kama sungura. Rangi yao ni kahawia au kijivu kwa kawaida lakini spishi nyingine zina rangi kali pia kama nyekundu au njano. Hula invertebrata kama wadudu, buibui, majongoo, tandu na nyunguyungu.

Spishi

Picha

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Sengi: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Sengi, njule au isanje ni wanyama wadogo wa familia Macroscelididae. Jina la njule litumika kwa jenasi Rhynchocyon na isanje litumika kwa Petrodromus tetradactylus. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika maeneo mbalimbali. Sifa bainifu mno ya sengi ni pua yao refu sana ambayo wanaweza kuipota ili kutafuta chakula. Hii inafanana kidogo na mwiro wa tembo na ni chimbuko cha jina lao la Kiingereza "elephant shrew". Miguu yao ni mirefu kwa kulinganisha na huenda wakirukaruka kama sungura. Rangi yao ni kahawia au kijivu kwa kawaida lakini spishi nyingine zina rangi kali pia kama nyekundu au njano. Hula invertebrata kama wadudu, buibui, majongoo, tandu na nyunguyungu.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri